SE7EP29 - SALAMA NA DEO GRATIUS | PRIVILEGED?!

Salama Na

Dec 29 2022 • 1 hr 11 mins

Deo Gratias, jina tu linatosha kujielezea kama wewe nawe utakua kama mimi wa kutaka kujua maana ya majina ya watu ili uweze kujua tabia zao au ujiulize wazee wake walikua wanafikiria nini wakati wanaamua kumpa jina hilo mtoto wao. Kwa Deo maana imejibeba na imejikamilisha na kwa yeye kuamua kubaki na jina lake hilo hilo mpaka kwenye stage ambako ndo sehemu yake ya kazi inabidi hilo nalo likuambie jambo kuhusu yeye na jinsi ambavyo anajichukulia na kuyachukulia mambo ambayo ameyachagua kuyafanya.

Shukrani ziende kwa Mungu ndo maana ya jina lake, shukrani ziende kwa Mungu kwa kila alifanyalo leo, shukrani ziende kwa Mungu maana baada ya wazee wake kumsomesha kwenye shule ambayo walikua wameianzisha wao na kuhakikisha kijana wao anapata elimu ambayo anastahili lakini yeye akaamua kuiacha fani ambayo aliisoma na kuamua kuwa mchekeshaji basi nadhani Shukrani ziende kwa Mungu, Shukrani ziende kwa Mungu kwa wazazi wake kuelewa, Shukrani pia ziende kwa Mungu kwasababu mwanga umeanza kuonekana kwenye lile alifanyalo sasa.

Yeye na rafiki zake ambao ni vijana wenzake wamejikusanya na kuanzisha kundi lao linaloitwa Watu Baki, ila hawakuamka tu wakaanzisha, kuna ka story hapo nyuma yake ambapo ndo panaleta maana kwenye maisha yetu na yao kama watafutaji. Deo anakumbuka audition ya kwanza ya Stand Up Comedy ambayo aliwahi kuifanya na akashinda huko Mbagala, chini ya shindano lililokua likisimamiwa na Evans Bukuku, Deo anakumbuka kushinda MILIONI nadhani kwenye shindano hilo ingawa alipofika home aligundua kuna mwana alichomoka na elfu kumi yake, yaani kuna mwana alimuangalia Deo, kisha akakiangalia kibunda alafu akasema nah, hawezi kumpa yote lol.

Courage ya kufanya mengine mengi ikiwa na pamoja na ambayo yanaendelea leo ilianzia hapo. Mengine yakabaki story!

Story ya kujikusanya na wanae enzi za Cheka Tu na baadae kuamua kundoka na kuanzisha WatuBaki ilikua mmoja inabidi awe na uthubutu na uthubutu huo uliwezekana na mpaka leo wamesimama na wana time yao kwenye DSTV ambayo inatoa burudani nzuri tu kwa watu wao na vile vile bado matamasha ya nje wanafanya wao kama wao.

Kwa wengi ikiwa pamoja na mimi tulipewa story kwamba Deo ni mtoto flani wa kishua alokua kutoka kwenye familia inayokula wali kwa kijiko na ndo maana baadhi ya mambo ilikua rahisi kwake kufanyika kwasababu ana uwezo wa kurudi nyumbani kwa Baba na Mama na akarudi na mzigo wa kutosha ambao unasaidia mambo yaende. Ila kwa mujibu wake, hiyo si habari na wala yeye hajatoka kwenye mazingira hayo ambayo wengi wanadhani ametokea.

Bado safari ndo kwanza imeanza na kwa wenzake yeye akiwa kama kiongozi anaamini kama wakitulia pamoja na kufuata maono yao basi mengi mazuri tu yatakuja, ila sasa huo uwezo wa kuweza kutulia pamoja na kutengeneza kitu kikubwa na kizuri ndo inawezakana ikawa mtihani. Si wengi wameweza ingawa wapo ambao wameanza pamoja na mpaka leo wanaunguruma pamoja. Inawezekana na yangu matumaini wao pia wataendelea kuwa WatuBaki kwa muda wote ulobaki.

Love,

Salama.

--- Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/yahstonetown/support

You Might Like

The Daily
The Daily
The New York Times
The Dan Bongino Show
The Dan Bongino Show
Cumulus Podcast Network | Dan Bongino
WSJ What’s News
WSJ What’s News
The Wall Street Journal
Pod Save America
Pod Save America
Crooked Media
Mark Levin Podcast
Mark Levin Podcast
Cumulus Podcast Network
Morning Joe
Morning Joe
Joe Scarborough and Mika Brzezinski, MSNBC
The Glenn Beck Program
The Glenn Beck Program
Blaze Podcast Network
The Rachel Maddow Show
The Rachel Maddow Show
Rachel Maddow, MSNBC
The Ben Shapiro Show
The Ben Shapiro Show
The Daily Wire
WSJ Your Money Briefing
WSJ Your Money Briefing
The Wall Street Journal
Morning Wire
Morning Wire
The Daily Wire
The Matt Walsh Show
The Matt Walsh Show
The Daily Wire
Serial
Serial
Serial Productions & The New York Times
The Fox News Rundown
The Fox News Rundown
FOX News Radio